01-Swalaah Ya Ijumaa Ni Fardhi Kwa Kila Mwanamme Haijuzu Kuiacha Kwa Sababu Ya Kazi Au Masomo n.k
Al-Lajnah Ad-Daaimah
Swalaah ya Ijumaa ni Fardhw ‘Ayn (Fardhi kwa kila mtu mwanamme) wala haijuzu kuiacha kwa sababu ya kazi au masomo na sababu kama hizo.
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):
“Na yeyote anayemcha Allaah; Atamjaalia njia ya kutoka (shidani).”