Shaykh 'Abdul-'Aziyz Aal Ash-Shaykh: Kupiga Punyeto Mchana Wa Mwezi Wa Ramadhwaan

SWALI:
 
Muuliza kutoka Canada anauliza, nimetoa Manii (punyeto) mchana wa Ramadhwaan hali ya kuwa nimefunga. Nifanye nini? 
 
JIBU:
 
(Alichofanya ni haraam) na ni juu yake alipe siku hio. Kwa kuwa kutoa manii kwa makusudi haijuzu. Allaah Anasema: "Mwenye kufunga anatakiwa kuacha chakula chake, kinywaji chake na matamanio yake kwa ajili Yangu".